Friday, August 24, 2007

HONGERA ASKOFU MALASUSA; VIJANA TUNAKUTARAJIA!

Hivi karibuni Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) lilifanya mkutano wake mkuu ambapo pia lilikuwa na uchaguzi wa Mkuu wa Kanisa hilo, baada ya aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo Askofu Dk. Samson Mushemba toka mwaka 1992 kumaliza muda wake. Katika mkutano huo, alichaguliwa Askofu Alex Gehazi Malasusa wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani yenye makao yake makuu Dar es salaam kuwa mkuu mpya wa Kanisa hilo kubwa hapa nchini baada ya Kanisa Katoliki. Kanisa hilo lina idadi ya Dayosisi ishirini hapa nchini na pia maeneo ya Misioni katika baadhi ya Mikoa na nchi jirani.

Kwanza sina budi kumshukuru sana Mungu kwa jinsi alivyoweka mkono wake katika mkutano huo mpaka wakampata mkuu mpya wa Kanisa hilo kwa amani, hasa kwa kuzingatia kuwa mwaka jana zoezi la kumpata mkuu huyo lilisshindikana kiasi cha kusababisha mchakato kuahirishwa kwa muda wa mwaka mmoja. Pili ninapenda kumpongeza sana Baba Askofu Malasusa kwa wajibu huo mzito aliokabidhiwa huku akiwa ni Askofu kijana kuliko maaskofu wengine ambao wamemzidi umri na hata elimu kwani wengine wana shahada ya Udaktari wa Falsafa (Phd) katika Theolojia. Mungu akuwezeshe kusimama imara katika wajibu wako huo ambao ni mzito lakini ni kwa msaada wake tu utauweza.

Pamoja na pongezi zangu hizo kwa Baba Askofu Malasusa, kimsingi nina mambo machache ya kumwelekeza kama changamoto kubwa katika wajibu wake ndani ya Kanisa hilo. Changamoto yangu ni juu ya hali ya vijana ndani ya taifa, jamii na madhehebu ya dini pia.

Kimsingi Baba Askofu Malasusa umechaguliwa kuwa kiongozi mkuu katika kipindi ambacho ni kigumu kiasi hasa kwa upande wa maisha ya vijana. Hii ni kutokana na kuwa vijana wa sasa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za kimaisha, ikiwemo suala la Utandawazi, ukosefu wa ajira katika sekta iliyo rasmi, mfumo wa elimu duni, hali ngumu ya maisha, mazingira magumu ya ufanyaji wa biashara, ukosefu wa mitaji na urasimu wa upatikanaji wa mitaji na mikopo ya kufanyia biashara, tatizo la matumizi ya dawa za kulevya, kasi ya maambukizo ya VVU/UKIMWI, na sualala mmomonyoko wa maadili ya vijana wetu. Nimependa kuzungumzia mambo haya kwa kuwa wewe kama kiongozi wa dini na mwenye wajibu wa kuwaongoza waumini wako katika hali ya kumfahamu na kumwishia Mungu, hata hivyo vijana ambao wanaishi katika mazingira haya magumu ya kimaisha, wanashindwa kusimama imara katika nafasi zao za kutumika katika madhehebu yetu ya kidini.

Hivyo ni wajibu wa wanajamii wote kuoni kwa namna gani wanaweza kushiriki katika wajibu wa kuwasaidia vijana ili waweze kusimama katika zamu zao kimaisha. Ninayasema haya kwa uchungu kwa kuwa nimeona kwa sehemu kubwa jinsi ambavyo vijana wamekuwa wakidharauliwa na kubezwa katika nafasi zao na hivyo kuonekana kuwa kama kitu kisicho na thamani yoyote kijamii. Vijana wamekata tamaa na kupoteza tumaini la maisha na ndio maana kila mara pamoja na mahubiri mazuri yanayotolewa katika nyumba zetu za ibada, badop vijana wetu wanaendelea kutenda maasi na mambo machafu na ya kutisha. Hata hivyo inawezekana kuwa viongozi wetu wa dini hamjafahamu ni nini kinahitajika kufanywa kwa vijana hao ili tuweze kuwaokoa katiak maangamizo makubwa yanayowakabili.Katika hilo ni lazima sote tujiulize sasa ni wajibu wa nani kufanya kitu kwa ajili ya maisha na malezi ya vijana.

Kama vile Katiba ya nchi yetu inavyoonyesha ni kuwa kuna mihimili mitatu inayoshirikiana katika utendaji wa kazi hapa nchini, mihimi hiyo ni Serikali, Bunge na Mahakama. Vivyo hivyo katika malezi ya vijana kuna mihimili mitatu inayopaswa kufanya kazi kwa pamoja. Mihimili hiyo ni Serikali, Jamii (Wazazi, walezi, waalimu n.k.) na Taasisi za dini. Mihimili yote hii inapofanya kazi yake inavyopasa, ndipo tutakapoona utendaji mzuri na wenye kuleta tija katika maisha ya vijana.

Sina uhakika kama ni viongozi wangapi wa kidini leo wanaofahamu juu ya hilo, lakini ni nafasi yangu hii naomba kuitumia kupitia kwako leo, kuwafikishia viongozi wengine ujumbe kutoka kwa vijana kuwa, sasa umefika wakati wa kuwafikia vijana. Hii ni kwa kuwa, vijana wamekuwa wakiumia, lakini hakuna wa kuwasaidia. Pamoja na kuwa kuna wajibu wa kiserikali, na wa kijamii, lakini nadhani makundi hayo mawili yamepoteza mwelekeo na hivyo hawajui ni nini wanaweza kufanya tena kwa ajili ya maisha ya vijana. Kwa kuwa hayo yameshindikana kwao, basi ni wajibu wenu kama walezi wetu wa kiroho, kuubeba wajibu huu ili kuokoa kizazi hiki kilichoharibika, ambacho Biblia inakiita kizazi cha nyoka. Ni vema madhehebu yote ya dini yakafahamu kuwa suala la kuwapatia vijana wetu ajira ni letu sote, suala la kuwapatia elimu vijana wetu ni letu sote, suala la kuwalea vijana katika maadili ya kitanzania ni letu sote, suala la kukemea kasi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana ni letu sote, suala la kusaidia kuondoa kasi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI ni letu sote. Hivyo hakuna ambaye atakwepa kubeba lawama kwa lolote litakalomtokea kijana wa leo wakati tuna nafasi ya kukemea, kuonya na kushauri hata kwa fimbo ikibidi.

Ni kweli kuwa Baba Askofu Malasusa umepewa wajibu huo ukiwa kijana mwenye nguvu, na Biblia inawasifu na kuwapongeza Vijana kuwa, “NIMEWAANDIKIA NINYI VIJANA, KWA KUWA MNA NGUVU NA NENO LA MUNGU LINAKAA NDANI YENU, NANYI MMEMSHINDA YULE MWOVU”! 1 Yohana 2:14b, hivyo hebu onyesha nguvu za ujana wako ili uweze kuwasaidia vijana hao waliopoteza matumaini yao chini ya jua hili. Huu ni wajibu mzito uliokabidhiwa, lakini Mungu mwenyewe ataenda kukuongoza na kukupigania katika wajibu huu.

Nimalizie kwa Neno linalosema kuwa, “EE BWANA, NIMESIKIA HABARI ZAKO NAMI NAOGOPA, EE BWANA FUFUA KAZI YAKO KATIKATI YA MIAKA. KATIKATI YA MIAKA TANGAZA HABARI YAKE. KATIKA GHADHABU KUMBUKA REHEMA”! Habakuki 3:2.

Mungu akuwezeshe ili uweze kusimamia ufufuo mpya wa kazi ya kuwalea Vijana ndani ya nje ya Taifa letu la Tanzania. Sisi pia tupo nyuma yako tukikuombea na kukutia moyo. Kuna mengi ya kukueleza Baba Askofu, lakini itoshe tu kwa mwanzo huu kusema kuwa mengine tutakueleza tukipata nafasi kwa kadri Mungu atakavyotujalia.

“Inuka! Maana shughuli hii yakuhusu wewe; na sisi tupo pamoja nawe. Uwe na moyo Mkuu! Ukaitende”! – Ezra 4:10.
Mungu Ibariki Tanzania! Mungu wabariki Vijana wa Tanzania!

Mwanaharakati wa masuala ya Vijana,

Hillary N. Mkony,
S.L.P. 743, Simu: 0754 – 000 215,
Barua pepe: hillarymy@yahoo.com
ARUSHA.

HONGERA KABWE: WEWE NI SHUJAA WA VIJANA!

Kwanza ninapenda kuwashukuru sana wasomaji wangu ambao walinipigia simu na wengine kunitumia ujumbe mfupi wa simu (sms), kunipongeza kwa makala yangu ya wiki iliyopita iliyokuwa na ujumbe kwa Rais Kikwete, iliyokuwa na kichwa, “Mhe. Kikwete Vijana wanasema hivi …….”! Kimsingi ninashukuru sana wote kwaniwalinipa moyo na changamoto kubwa kwangu juu ya wajibu wangu wa kuwasemea vijana. Ahsanteni sana na ninaomba mzidi kunishauri kila mara.

Wiki iliyopita, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilimsimamisha kuhudhuria vikao vya mikutano miwili ya bunge hilo, Mhe. Zitto Zubeir Kabwe kwa madai ya kusema uongo bungeni. Katika hatua hiyo ambayo imepokelewa kwa mitazamo tofauti na wananchi, wanajamii, wanasheria, wasomi na wanaharakati mbalimbali hapa nchini. Kimsingi kulikuwa kunahitajika mafafanuzi ya hali juu kutokana na hatua hiyo ambayo imeonekana kuwa bunge hilo limetumika kama chambo katika kuminya demokrasia badala ya kuijenga na kuitetea. Kwa sehemu kubwa kumekuwa na kauli kutoka kwa watu mbalimbali juu ya hatua hiyo ya kusimamishwa kwa Mhe. Kabwe. Hata hivyo nami kama mmoja wa wadau wa vijana na mwanaharakati, nitapenda kuongelea jambo kwa sehemu tu juu ya suala hilo. Hata hivyo mimi nitapenda kuliongelea suala hilo kwa mtazamo wa tofauti hasa kwa kuzingatia kuwa Zitto ni sehemu ya vijana na kwa hivyo jambo analolifanya kama mbunge, pia linawagusa vijana ambao yeye ni mwakilishi wao katika chombo hicho cha kutunga sheria. Hivyo nitapenda kuzungumzia juu ya nafasi na wajibu ambao umeendwa kuonyeshwa na mbunge huyo kijana ambaye bado ana nafasi kubwa ya kuwatumikia wapiga kura wake na watanzania kwa ujumla.

Kwa sehemu kubwa sisi kama wapiga kura wa Tanzania tunafahamu kuwa tuna wabunge wetu wanaotuwakilisha katika chombo hicho cha kutunga sheria, hata hivyo kwa sehemu kubwa tumekuwa tukishuhudia juu ya wengi wa wawakilishi wetu hao kushindwa kutumia nafasi na wajibu tuliyowapa kama wapiga kura wao na badala yake kubaki wakishabikia masuala ya vyama vyao bungeni. Kwa hali hii ndipo sisi kama wapiga kura tumekuwa tukijiuliza, ndicho tulichowatuma muende mkafanye bungeni? Mbona kuna mambo mengi ambayo ni ya msingi na yanahitaji kuzungumzwa na wabunge wetu na hivyo kupatiwa majibu toka serikalini. Sasa waheshimiwa mnapoacha kutekeleza wajibu huo ulio muhimu kwenu na kuamua kuwa wajibu hoja kwa niaba ya serikali, kwa hali hiyo mwataka tuwaeleweje? Ni vema mkafahamu kuwa mmepewa wajibu wa kuwakilisha hoja na haja za wapiga kura wenu serikalini kupitia katika bunge.

Mara kwa mara nimekuwa nikifuatilia na kutazama juu ya nafasi za vijana katika wajibu wa kuwatumikia wananchi hapa nchini na pengine duniani. Kimsingi nimesoma katika historia juu ya vijana wengi ambao walikubali kuwa wawakilishi wa watu na hata wengine kufikia mahali pa kukubali kutoa kafara maisha yao. Miongoni mwao ni pamoja Mwanaharakati wa ukombozi Afrika Kusini marehemu Steve Biko ambaye aliuwawa na makaburu akiwa na miaka 30. Wengine ni pamoja Yesu Kristo ambaye alimua kuyatoa maisha yake kwa ajili ya wanadamu wote na hatimaye kuuwawa kwa kuangikwa msalabani akiwa na miaka 33. Pia katika msahafu wa Kikristo (Biblia), tunasoma juu ya kijana mwingine ambaye aliweza kulinda na kutetea nafasi yake kama kijana ndani ya jamii, kijana aliitwa Yusufu, ambaye aliukuwa ni mtumishi katika jumba la Kiongozi wa jeshi la Kimisri ambaye alikuwa anaitwa Potifa. Mke wa Potifa alikuwa anamtaka Yusufu ili aweze kufanya naye ngono, lakini yeye (Yusufu) alikataa na kuamua kukimbia na hata kumuachia nguo yake, jambo hili lilikuwa ni gumu kwani lilimgharimu Yusufu kiasi cha kufungwa gerezani. Lakini aliilinda heshima na hadhi yake na pia kumheshimu Mungu wake. Hawa ni sehemu tu ya mifano ya watu ambao walikuwa ni vijana lakini walikuwa tayari kupoteza maisha yao kwa ajili ya wengi. Nimeona niitumie mifano hii kwa kuonyesha jinsi ambavyo Mhe. Zitto Kabwe alivyokubali kutumia nafasi yake kama kijana na mwakilishi wetu kutetea maisha na uchumi wa watanzania. Ninakiri kuwa katika mazingira ya sasa ni watu wachache sana ambao wana roho na moyo kama wa Kabwe. Hii ni kwa kuwa wakati wa kchukua hatua za kumuadhibu bungeni, pamoja na kupewa nafasi na kutakiwa kujitetea yeye aliishia kwa kusema kuwa, yeye ni mwanademokrasia, hivyo yupo tayari kwa lolote.

Kwa tukio hili la Mhe. Kabwe linaonyesha jinsi yeye kama mwakilishi wa wapiga kura na kama kijana alivyo na uchungu na upendo kwa nchi yake Tanzania. Hivyo hakuona shida kukubali kusimamishwa kujihusisha na shughuli za bunge huku akipokea nusu mshahara kwa kipindi cha miezi mitano. Naomba ieleweke wazi kuwa, iwapo tungekuwa na wabunge wengi wenye moyo kama wa Mhe. Kabwe, basi kwa sehemu kubwa nchi yetu ingekuwa imetoka kwenye matatizo magumu yaliyopo. Yapo mambo mengi yanayotokea, ambayo yamekuwa ni matatizo makubwa kwa wananchi na vijana wa Tanzania, lakini ni nani anaweza kuyawakisilisha mbele ya serikali au hata kukemea, inaonekana hakuna, wengi wapo kwa ajili ya maslahi yao tu. Mara kwa mara nimekuwa nikijiuliza bila kupata majibu, kuna ni nani nabii mpya wa Tanzania, mbona wale tuliokuwa tunawatarajia ndio hao wametutosa na kutuacha kwenye mataa, hatujui ni wapi pa kukimbilia kwani kote huko kumekuwa ni pabaya zaidi ya matarajio yetu. Hapo ndipo ninaposhindwa kuelewa kama kweli waliopo madarakani sasa ni wale tuliokuwa tunawatarajia au kuna wengine tuwasubiri.

Mambo mengi yanawakabili watanzania na hususan vijana, lakini wale ambao leo ndio tunawaita waheshimiwa wawakilishi wetu, wamekaa kimya kama vile mambo hayo hayawahusu, wamekuwa tayari kuacha sisi tufe ili mradi wao wanapokea maslahi yao makubwa kila iitwapo leo. Tazama jinsi tatizo la dawa za kulevya linavyowaangamiza vijana, tazama kasi ya maambukizo ya VVU/UKIMWI ilivyo hapa nchini, tazama suala umasikini unavyowakabili watanzania wengi, tazama hali ya ukosefu wa ajira, elimu nzuri na hata fursa nzuri za kufanya biashara hakuna, tatizo la ukosefu wa mitaji au hata mikopo ni kubwa kwa jamii, yote haya ni sehemu ya mambo yanayowakabili watanzania, lakini hakuna anayeyaona, wote wapo kwa ajili ya maslahi yao. Kwa hali hii tunao wawakilishi kweli?

Kinachoonekana katika suala hili la Mhe. Kabwe pamoja na mambo mengi yanayotokea katika bunge letu hili ambalo kinara wake aliahidi kuliongoza kwa VIWANGO NA KASI, ni katika hali ya kulinda maslahi ya Chama, wawakilishi wetu wengi hawana uchungu na maslahi ya taifa letu la Tanzania, bali wana maslahi na matumbo yao na Vyama vyao tu. Naomba ieleweke kuwa kama kweli Bunge letu na waheshimiwa wabunge wangekuwa na maslahi na Tanzania, wangemsikiliza mbunge mwenzao na kuipitisha hoja yake ili kuweza kumchunguza Mhe. Waziri Karamagi, lakini kwa kuwa hawana maslahi na Tanzania ndio maana waliamua kumsulubu mwenzao Kabwe. Hapo ndipo ninapojiuliza, ni lini watakapopatikana wawakilishi wenye uchungu na maslahi na Tanzania.

Nimalizie kwa kumtia moyo Mhe. Kabwe kuwa yeye ni sehemu tu ya watu walioonyesha hali ya kuthubutu kusema, jambo uthubutu wake umemgharimu, lakini afahamu kuwa hiyo ni gharama ya kuwa MKWELI. Kama alivyosema Mwanafalsafa Steve Biko kuwa “HERI KUFA UKIWA NA KAULI INAYOISHI, KULIKO KUISHI UKIWA HUNA KAULI”! Hivyo Mhe. Kabwe usikate tamaa, tumekuona ukweli wako na ulivyokugharimu, tumefahamu kuwa u shujaa wetu sisi Vijana, wewe songa mbele na sisi TUPO NYUMA YAKO, tunakufuata. Umetuonyesha mwanga mpya vijana na hivyo tuna wajibu wa kuufuata, usikatishwe tamaa na hayo, wewe ni kamanda, nyuma yako lipo jeshi kubwa la Vijana, Tunasubiri kauli yako.

Mungu Ibariki Tanzania! Mungu Wabariki Vijana wa Tanzania!

Mwanaharakati wa Masuala ya Vijana,

Hillary N. Mkony,
S.L.P. 743, Simu: 0754-000215,
Barua pepe: hillarymy@yahoo.com
ARUSHA.

HONGERA KABWE: WEWE NI SHUJAA WA VIJANA!

Kwanza ninapenda kuwashukuru sana wasomaji wangu ambao walinipigia simu na wengine kunitumia ujumbe mfupi wa simu (sms), kunipongeza kwa makala yangu ya wiki iliyopita iliyokuwa na ujumbe kwa Rais Kikwete, iliyokuwa na kichwa, “Mhe. Kikwete Vijana wanasema hivi …….”! Kimsingi ninashukuru sana wote kwaniwalinipa moyo na changamoto kubwa kwangu juu ya wajibu wangu wa kuwasemea vijana. Ahsanteni sana na ninaomba mzidi kunishauri kila mara.

Wiki iliyopita, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilimsimamisha kuhudhuria vikao vya mikutano miwili ya bunge hilo, Mhe. Zitto Zubeir Kabwe kwa madai ya kusema uongo bungeni. Katika hatua hiyo ambayo imepokelewa kwa mitazamo tofauti na wananchi, wanajamii, wanasheria, wasomi na wanaharakati mbalimbali hapa nchini. Kimsingi kulikuwa kunahitajika mafafanuzi ya hali juu kutokana na hatua hiyo ambayo imeonekana kuwa bunge hilo limetumika kama chambo katika kuminya demokrasia badala ya kuijenga na kuitetea. Kwa sehemu kubwa kumekuwa na kauli kutoka kwa watu mbalimbali juu ya hatua hiyo ya kusimamishwa kwa Mhe. Kabwe. Hata hivyo nami kama mmoja wa wadau wa vijana na mwanaharakati, nitapenda kuongelea jambo kwa sehemu tu juu ya suala hilo. Hata hivyo mimi nitapenda kuliongelea suala hilo kwa mtazamo wa tofauti hasa kwa kuzingatia kuwa Zitto ni sehemu ya vijana na kwa hivyo jambo analolifanya kama mbunge, pia linawagusa vijana ambao yeye ni mwakilishi wao katika chombo hicho cha kutunga sheria. Hivyo nitapenda kuzungumzia juu ya nafasi na wajibu ambao umeendwa kuonyeshwa na mbunge huyo kijana ambaye bado ana nafasi kubwa ya kuwatumikia wapiga kura wake na watanzania kwa ujumla.

Kwa sehemu kubwa sisi kama wapiga kura wa Tanzania tunafahamu kuwa tuna wabunge wetu wanaotuwakilisha katika chombo hicho cha kutunga sheria, hata hivyo kwa sehemu kubwa tumekuwa tukishuhudia juu ya wengi wa wawakilishi wetu hao kushindwa kutumia nafasi na wajibu tuliyowapa kama wapiga kura wao na badala yake kubaki wakishabikia masuala ya vyama vyao bungeni. Kwa hali hii ndipo sisi kama wapiga kura tumekuwa tukijiuliza, ndicho tulichowatuma muende mkafanye bungeni? Mbona kuna mambo mengi ambayo ni ya msingi na yanahitaji kuzungumzwa na wabunge wetu na hivyo kupatiwa majibu toka serikalini. Sasa waheshimiwa mnapoacha kutekeleza wajibu huo ulio muhimu kwenu na kuamua kuwa wajibu hoja kwa niaba ya serikali, kwa hali hiyo mwataka tuwaeleweje? Ni vema mkafahamu kuwa mmepewa wajibu wa kuwakilisha hoja na haja za wapiga kura wenu serikalini kupitia katika bunge.

Mara kwa mara nimekuwa nikifuatilia na kutazama juu ya nafasi za vijana katika wajibu wa kuwatumikia wananchi hapa nchini na pengine duniani. Kimsingi nimesoma katika historia juu ya vijana wengi ambao walikubali kuwa wawakilishi wa watu na hata wengine kufikia mahali pa kukubali kutoa kafara maisha yao. Miongoni mwao ni pamoja Mwanaharakati wa ukombozi Afrika Kusini marehemu Steve Biko ambaye aliuwawa na makaburu akiwa na miaka 30. Wengine ni pamoja Yesu Kristo ambaye alimua kuyatoa maisha yake kwa ajili ya wanadamu wote na hatimaye kuuwawa kwa kuangikwa msalabani akiwa na miaka 33. Pia katika msahafu wa Kikristo (Biblia), tunasoma juu ya kijana mwingine ambaye aliweza kulinda na kutetea nafasi yake kama kijana ndani ya jamii, kijana aliitwa Yusufu, ambaye aliukuwa ni mtumishi katika jumba la Kiongozi wa jeshi la Kimisri ambaye alikuwa anaitwa Potifa. Mke wa Potifa alikuwa anamtaka Yusufu ili aweze kufanya naye ngono, lakini yeye (Yusufu) alikataa na kuamua kukimbia na hata kumuachia nguo yake, jambo hili lilikuwa ni gumu kwani lilimgharimu Yusufu kiasi cha kufungwa gerezani. Lakini aliilinda heshima na hadhi yake na pia kumheshimu Mungu wake. Hawa ni sehemu tu ya mifano ya watu ambao walikuwa ni vijana lakini walikuwa tayari kupoteza maisha yao kwa ajili ya wengi. Nimeona niitumie mifano hii kwa kuonyesha jinsi ambavyo Mhe. Zitto Kabwe alivyokubali kutumia nafasi yake kama kijana na mwakilishi wetu kutetea maisha na uchumi wa watanzania. Ninakiri kuwa katika mazingira ya sasa ni watu wachache sana ambao wana roho na moyo kama wa Kabwe. Hii ni kwa kuwa wakati wa kchukua hatua za kumuadhibu bungeni, pamoja na kupewa nafasi na kutakiwa kujitetea yeye aliishia kwa kusema kuwa, yeye ni mwanademokrasia, hivyo yupo tayari kwa lolote.

Kwa tukio hili la Mhe. Kabwe linaonyesha jinsi yeye kama mwakilishi wa wapiga kura na kama kijana alivyo na uchungu na upendo kwa nchi yake Tanzania. Hivyo hakuona shida kukubali kusimamishwa kujihusisha na shughuli za bunge huku akipokea nusu mshahara kwa kipindi cha miezi mitano. Naomba ieleweke wazi kuwa, iwapo tungekuwa na wabunge wengi wenye moyo kama wa Mhe. Kabwe, basi kwa sehemu kubwa nchi yetu ingekuwa imetoka kwenye matatizo magumu yaliyopo. Yapo mambo mengi yanayotokea, ambayo yamekuwa ni matatizo makubwa kwa wananchi na vijana wa Tanzania, lakini ni nani anaweza kuyawakisilisha mbele ya serikali au hata kukemea, inaonekana hakuna, wengi wapo kwa ajili ya maslahi yao tu. Mara kwa mara nimekuwa nikijiuliza bila kupata majibu, kuna ni nani nabii mpya wa Tanzania, mbona wale tuliokuwa tunawatarajia ndio hao wametutosa na kutuacha kwenye mataa, hatujui ni wapi pa kukimbilia kwani kote huko kumekuwa ni pabaya zaidi ya matarajio yetu. Hapo ndipo ninaposhindwa kuelewa kama kweli waliopo madarakani sasa ni wale tuliokuwa tunawatarajia au kuna wengine tuwasubiri.

Mambo mengi yanawakabili watanzania na hususan vijana, lakini wale ambao leo ndio tunawaita waheshimiwa wawakilishi wetu, wamekaa kimya kama vile mambo hayo hayawahusu, wamekuwa tayari kuacha sisi tufe ili mradi wao wanapokea maslahi yao makubwa kila iitwapo leo. Tazama jinsi tatizo la dawa za kulevya linavyowaangamiza vijana, tazama kasi ya maambukizo ya VVU/UKIMWI ilivyo hapa nchini, tazama suala umasikini unavyowakabili watanzania wengi, tazama hali ya ukosefu wa ajira, elimu nzuri na hata fursa nzuri za kufanya biashara hakuna, tatizo la ukosefu wa mitaji au hata mikopo ni kubwa kwa jamii, yote haya ni sehemu ya mambo yanayowakabili watanzania, lakini hakuna anayeyaona, wote wapo kwa ajili ya maslahi yao. Kwa hali hii tunao wawakilishi kweli?

Kinachoonekana katika suala hili la Mhe. Kabwe pamoja na mambo mengi yanayotokea katika bunge letu hili ambalo kinara wake aliahidi kuliongoza kwa VIWANGO NA KASI, ni katika hali ya kulinda maslahi ya Chama, wawakilishi wetu wengi hawana uchungu na maslahi ya taifa letu la Tanzania, bali wana maslahi na matumbo yao na Vyama vyao tu. Naomba ieleweke kuwa kama kweli Bunge letu na waheshimiwa wabunge wangekuwa na maslahi na Tanzania, wangemsikiliza mbunge mwenzao na kuipitisha hoja yake ili kuweza kumchunguza Mhe. Waziri Karamagi, lakini kwa kuwa hawana maslahi na Tanzania ndio maana waliamua kumsulubu mwenzao Kabwe. Hapo ndipo ninapojiuliza, ni lini watakapopatikana wawakilishi wenye uchungu na maslahi na Tanzania.

Nimalizie kwa kumtia moyo Mhe. Kabwe kuwa yeye ni sehemu tu ya watu walioonyesha hali ya kuthubutu kusema, jambo uthubutu wake umemgharimu, lakini afahamu kuwa hiyo ni gharama ya kuwa MKWELI. Kama alivyosema Mwanafalsafa Steve Biko kuwa “HERI KUFA UKIWA NA KAULI INAYOISHI, KULIKO KUISHI UKIWA HUNA KAULI”! Hivyo Mhe. Kabwe usikate tamaa, tumekuona ukweli wako na ulivyokugharimu, tumefahamu kuwa u shujaa wetu sisi Vijana, wewe songa mbele na sisi TUPO NYUMA YAKO, tunakufuata. Umetuonyesha mwanga mpya vijana na hivyo tuna wajibu wa kuufuata, usikatishwe tamaa na hayo, wewe ni kamanda, nyuma yako lipo jeshi kubwa la Vijana, Tunasubiri kauli yako.

Mungu Ibariki Tanzania! Mungu Wabariki Vijana wa Tanzania!

Mwanaharakati wa Masuala ya Vijana,

Hillary N. Mkony,
S.L.P. 743, Simu: 0754-000215,
Barua pepe: hillarymy@yahoo.com
ARUSHA.

BURIANI AMINA CHIFUPA; VIJANA TUMEKUSIKIA!



Wiki hii taifa la Tanzania hususan jamii ya Vijana lilikumbwa na msiba mzito wa kuondokewa na Mbunge wa Viti Maalum (UV-CCM), Mhe. Amina Chifupa Mpakanjia aliyefariki tarehe 26.06.2007, baada ya kuugua kwa muda mfupi. Kimsingi msiba huu ni pigo kubwa sana kwa wanajamii wote na hasa sisi tulio katika mapambano ya kuwakomboa Vijana.

Mhe. Amina tulifahamiana kwa muda mfupi sana lakini kwa kipindi hicho kifupi, niligundua ni mtu mwenye msimamo usioyumba. Mwezi July, mwaka jana, niliandika makala kwenye gazeti hili juu ya Amina makala iliyokuwa na kichwa: “HONGERA MHE. CHIFUPA; WABUNGE WENGINE VIJANA MPO WAPI?” Baada ya makala hiyo nilipokea simu toka kwa waheshimiwa wabunge na mawaziri mbalimbali akiwemo Marehemu Amina mwenyewe, tulizungumza mengi na kuweza kuonana na tokea hapo, ndipo tulipozidi kuwa na ukaribu ulionifanya niweze kumfahamu Mhe.Amina kwa kiasi fulani.

Kwa kipindi kifupi nilichomfahamu Marehemu Amina, kimsingi nilijifunza mengi, hivyo leo nina ujasiri wa kumuandika na kusema kweli safari yake fupi hapa duniani haikuwa ni ya hasara, Marehemu Amina ameondoka kijasiri, Amekufa kishujaa. Amina amelala lakini bado fikra, mwelekeo, malengo, na kauli zake bado zinaishi na zitaishi milele yote. Ninakumbuka wakati alipokuwa anagombea Ubunge kupitia Jumuiya ya Vijana (UVCCM), jinsi ambavyo alikumbana na vikwazo mbalimbali kutoka kwa watu tofauti, wengine walidiriki hata kumuandika kwenye vyombo vya habari waziwazi wakimbeza na kumkashifu kuwa hafai kuwa mbunge, lakini yeye alisimama kidete na kulinda heshima na hadhi yake na hatimaye alifanikiwa kuvuka vikwazo hivyo na kuwa Mbunge mwenye umri mdogo kuliko wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata baada ya kuingia bungeni, Mhe Amina hakuwa kimya kama wengi walivyodhani, bali alisimama imara na kuonesha wazi nia na wajibu uliompeleka bungeni wa kuwatetea Vijana. Hivyo leo tunasikia Amina amefariki, tunajua wazi kuwa Vijana tumempoteza mwakilishi wetu hodari na aliyekuwa na nia ya kutusaidia.

Uwakilishi wa Mhe. Amina haukuishia kuchangia mijadala kwenye vikao vya Bunge tu, bado tulimsikia na kumuona akifanya shughuli mbalimbali za kijamii, kama kuwatembea vijana na watoto wenye matatizo mbalimbali, kwa hili tuliona jinsi Mhe. Amina alivyokuwa na moyo wa kuwatumikia Vijana na wanajamii wa Kitanzania.

Pamoja na kumkumbuka Mhe. Amina, ni vema sisi kama Vijana na wanajamii tukajiuliza ni kitu gani tumejifunza kutoka kwake, je ni jambo gani tutakalomkumbuka nalo maishani mwetu. Mimi binafsi kama Mwanaharakati na mdau wa masuala ya Vijana, nimejifunza mambo mengi kutoka kwa marehemu Amina na mambo hayo ni chamamoto kubwa kwangu katika wajibu na nafasi yangu ya kuwatumikia Vijana. Ninaomba niwakumbushe vijana na wanajamii mambo machache niliyojifunza kutoka kwa Mpendwa wetu huyu.

Amina alikuwa ni mwanaharakati, mpambanaji na mwakilishi mwenye nia na mikakati mingi na mizuri kwa ajili ya vijana siku za mbeleni. Mapambano ya Amina dhidi ya matatizo ya vijana na hususan suala la matumizi ya dawa za kulevya ni sehemu tu ya vitu ambavyo vilimjengea heshima kubwa kwa jamii na vijana na wote wenye mapenzi mema na maisha ya vijana hapa nchini. Ninakumbuka alisema kuwa yupo tayari kufa kwa ajili ya kuwatetea vijana wanaokabiliwa na matatizo mengi ya ukosefu wa kazi, elimu duni, ukosefu wa maeneo huru ya kufanyia biashara na suala la mmomonyoko wa maadili.

Marehemu Amina alikuwa ni kijana mwenye nia na malengo ya kufika mbali, hii ni pamoja na kusimama kwake kidete akilinda na kutetea nafasi yake kwa wale wote waliokuwa na nia ya kumkwamisha na kumrudisha nyuma, Amina alifahamu umuhimu wa elimu na ndio maana mpaka wakati anafariki licha ya kuwa alikuwa ni Mbunge, bado alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).

Mambo haya na mengine mengi yanamfanya Amina awe kioo kwetu kama Vijana na wanajamii wengine. Ninapenda kuwakumbusha wapendwa kuwa, katika kumuenzi na kumkumbuka Marehemu Amina ni wajibu wetu kusimama katika mstari ule aliosimama na kuutetea siku zote. Kwa waheshimiwa wabunge hususan wabunge vijana, mnapaswa kufahamu kuwa mna wajibu mzito wa kuwatetea vijana wenzenu bungeni na pia katika maeneo mbalimbali mnayoweza kuyafikia. Zaidi kuzidisha mapambano juu ya tatizo la dawa za kulevya ili vita hii ambayo Mhe. Amina aliipigania hadi siku ya umauti wake iweze kushinda na vijana wakombolewe katika hilo.

Kwa wapendwa vijana wenzangu, Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye ujasiri wa kupigania haki yake na hadhi aliyonayo kijamii, hivyo ni wajibu wetu leo kama Vijana kuhakikisha kuwa na sisi tunatetea na kulinda hadhi yetu kijamii, hadhi hii inapaswa kulindwa hata ikibidi kufa, lakini tusikubali mtu awaye yote atudhalilishe na kutudharau eti kwa kuwa sisi ni vijana. Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye kutafuta elimu, hivyo ni wajibu na nafasi yetu kama vijana kuhakikisha kuwa na sisi tunaitafuta sana elimu bila kujali kiwango cha elimu tuliyo nayo sasa, tuhakikishe kuwa maadamu tunaishi tunasoma hadi mwisho wa maisha yetu. Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye kuishi bila makuu licha ya ubunge wake. Hayo ni mambo ambayo sisi kama Vijana tunapaswa kuyaiga toka kwa marehemu Amina na kuyaenzi yale yote aliyoyaacha kwetu.

Wiki hii katika makala yangu, nilipanga kuandika tena juu ya suala la dawa za kulevya hasa ukizingatia kuwa ilikuwa ni wiki ya maadhimisho ya kupiga vita na kudhibiti matumizi ya dawa hizo. Hata hivyo suala la hilo nililiacha baada ya kusikia habari za msiba huu wa kusikitisha wa Mpendwa wetu Amina Chifupa Mpakanjia (Mbunge wa Vijana), sijui kama wengi tunalifahamu hili, lakini ni kuwa Marehemu Amina alikuwa anapigania sana suala la athari za matumizi ya dawa za kulevya kwa Vijana. Kwa neema, Mungu amemchukua Amina siku ya kilele cha kupambana na dawa za kulevya na siku hiyo (26.06.07), Mhe. Rais Jakaya Kikwete alikuwa Mjini Tanga kwenye maadhimisho ya siku hiyo ya kupambana na dawa hizo za kulevya. Hivyo Amina alikuwa ni Mpiganaji wa kweli katika tatizo hili, na hata Mungu anajua.

Mwanaharakati wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, marehemu Steve Biko aliyeuwawa kinyama na makaburu mwaka 1978 akiwa kijana mdogo, alikufa akiwa na falsafa hii, “HERI KUFA UKIWA NA KAULI INAYOISHI; KULIKO KUISHI UKIWA HUNA KAULI!”. Nimeikumbuka falsafa hii baada ya kifo cha Mhe. Amina. Ni kweli kuwa Amina amekufa, Amina amelala na wala hatutakaa tumuone tena katika maisha ya kibinadamu, lakini kauli zake zinaishi na kauli hizi zitaishi hata mwisho wa dunia. Hivyo Mpendwa Amina ninapenda kusema, VIJANA TULIKUPENDA, LAKINI MUNGU ALIKUPENDA ZAIDI, NENDA KAPUMZIKE DADA, LAKINI FAHAMU KUWA SISI KAMA VIJANA NA WANAJAMII TUNAKUMBUKA NA KUENZI MAMBO YOTE MAZURI ULIYOYAACHA!

Msahafu wa Kikristo (Biblia) unassema, “MTU AWAYE YOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO, BALI UWE KIELELEZO KWAO WAAMINIO, KATIKA USEMI, KATIKA MWENENDO, KATIKA UPENDO, NA KATIK AIMANI NA USAFI! –2 Timotheo 4:12–13.

Kweli Amina umelinda heshima ya Ujana wako na ndio maana sisi tunasema kuwa, tumejifunza kutoka kwako kuwa, kuishi bila kauli ni mbaya, heri kufa ukiwa na kauli inayoishi. Mwenyezi Mungu aipumzishe Roho yako mahali pema peponi, Upumzike kwa Amani.

Mungu Ibariki Tanzania! Mungu wabariki Vijana wa Tanzania!

Hillary N. Mkony,
Mwanaharakati wa masuala ya Vijana,
S.L.P. 743, Simu: 0754 000 215,
ARUSHA.

BURIANI AMINA CHIFUPA; VIJANA TUMEKUSIKIA!



Wiki hii taifa la Tanzania hususan jamii ya Vijana lilikumbwa na msiba mzito wa kuondokewa na Mbunge wa Viti Maalum (UV-CCM), Mhe. Amina Chifupa Mpakanjia aliyefariki tarehe 26.06.2007, baada ya kuugua kwa muda mfupi. Kimsingi msiba huu ni pigo kubwa sana kwa wanajamii wote na hasa sisi tulio katika mapambano ya kuwakomboa Vijana.

Mhe. Amina tulifahamiana kwa muda mfupi sana lakini kwa kipindi hicho kifupi, niligundua ni mtu mwenye msimamo usioyumba. Mwezi July, mwaka jana, niliandika makala kwenye gazeti hili juu ya Amina makala iliyokuwa na kichwa: “HONGERA MHE. CHIFUPA; WABUNGE WENGINE VIJANA MPO WAPI?” Baada ya makala hiyo nilipokea simu toka kwa waheshimiwa wabunge na mawaziri mbalimbali akiwemo Marehemu Amina mwenyewe, tulizungumza mengi na kuweza kuonana na tokea hapo, ndipo tulipozidi kuwa na ukaribu ulionifanya niweze kumfahamu Mhe.Amina kwa kiasi fulani.

Kwa kipindi kifupi nilichomfahamu Marehemu Amina, kimsingi nilijifunza mengi, hivyo leo nina ujasiri wa kumuandika na kusema kweli safari yake fupi hapa duniani haikuwa ni ya hasara, Marehemu Amina ameondoka kijasiri, Amekufa kishujaa. Amina amelala lakini bado fikra, mwelekeo, malengo, na kauli zake bado zinaishi na zitaishi milele yote. Ninakumbuka wakati alipokuwa anagombea Ubunge kupitia Jumuiya ya Vijana (UVCCM), jinsi ambavyo alikumbana na vikwazo mbalimbali kutoka kwa watu tofauti, wengine walidiriki hata kumuandika kwenye vyombo vya habari waziwazi wakimbeza na kumkashifu kuwa hafai kuwa mbunge, lakini yeye alisimama kidete na kulinda heshima na hadhi yake na hatimaye alifanikiwa kuvuka vikwazo hivyo na kuwa Mbunge mwenye umri mdogo kuliko wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata baada ya kuingia bungeni, Mhe Amina hakuwa kimya kama wengi walivyodhani, bali alisimama imara na kuonesha wazi nia na wajibu uliompeleka bungeni wa kuwatetea Vijana. Hivyo leo tunasikia Amina amefariki, tunajua wazi kuwa Vijana tumempoteza mwakilishi wetu hodari na aliyekuwa na nia ya kutusaidia.

Uwakilishi wa Mhe. Amina haukuishia kuchangia mijadala kwenye vikao vya Bunge tu, bado tulimsikia na kumuona akifanya shughuli mbalimbali za kijamii, kama kuwatembea vijana na watoto wenye matatizo mbalimbali, kwa hili tuliona jinsi Mhe. Amina alivyokuwa na moyo wa kuwatumikia Vijana na wanajamii wa Kitanzania.

Pamoja na kumkumbuka Mhe. Amina, ni vema sisi kama Vijana na wanajamii tukajiuliza ni kitu gani tumejifunza kutoka kwake, je ni jambo gani tutakalomkumbuka nalo maishani mwetu. Mimi binafsi kama Mwanaharakati na mdau wa masuala ya Vijana, nimejifunza mambo mengi kutoka kwa marehemu Amina na mambo hayo ni chamamoto kubwa kwangu katika wajibu na nafasi yangu ya kuwatumikia Vijana. Ninaomba niwakumbushe vijana na wanajamii mambo machache niliyojifunza kutoka kwa Mpendwa wetu huyu.

Amina alikuwa ni mwanaharakati, mpambanaji na mwakilishi mwenye nia na mikakati mingi na mizuri kwa ajili ya vijana siku za mbeleni. Mapambano ya Amina dhidi ya matatizo ya vijana na hususan suala la matumizi ya dawa za kulevya ni sehemu tu ya vitu ambavyo vilimjengea heshima kubwa kwa jamii na vijana na wote wenye mapenzi mema na maisha ya vijana hapa nchini. Ninakumbuka alisema kuwa yupo tayari kufa kwa ajili ya kuwatetea vijana wanaokabiliwa na matatizo mengi ya ukosefu wa kazi, elimu duni, ukosefu wa maeneo huru ya kufanyia biashara na suala la mmomonyoko wa maadili.

Marehemu Amina alikuwa ni kijana mwenye nia na malengo ya kufika mbali, hii ni pamoja na kusimama kwake kidete akilinda na kutetea nafasi yake kwa wale wote waliokuwa na nia ya kumkwamisha na kumrudisha nyuma, Amina alifahamu umuhimu wa elimu na ndio maana mpaka wakati anafariki licha ya kuwa alikuwa ni Mbunge, bado alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).

Mambo haya na mengine mengi yanamfanya Amina awe kioo kwetu kama Vijana na wanajamii wengine. Ninapenda kuwakumbusha wapendwa kuwa, katika kumuenzi na kumkumbuka Marehemu Amina ni wajibu wetu kusimama katika mstari ule aliosimama na kuutetea siku zote. Kwa waheshimiwa wabunge hususan wabunge vijana, mnapaswa kufahamu kuwa mna wajibu mzito wa kuwatetea vijana wenzenu bungeni na pia katika maeneo mbalimbali mnayoweza kuyafikia. Zaidi kuzidisha mapambano juu ya tatizo la dawa za kulevya ili vita hii ambayo Mhe. Amina aliipigania hadi siku ya umauti wake iweze kushinda na vijana wakombolewe katika hilo.

Kwa wapendwa vijana wenzangu, Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye ujasiri wa kupigania haki yake na hadhi aliyonayo kijamii, hivyo ni wajibu wetu leo kama Vijana kuhakikisha kuwa na sisi tunatetea na kulinda hadhi yetu kijamii, hadhi hii inapaswa kulindwa hata ikibidi kufa, lakini tusikubali mtu awaye yote atudhalilishe na kutudharau eti kwa kuwa sisi ni vijana. Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye kutafuta elimu, hivyo ni wajibu na nafasi yetu kama vijana kuhakikisha kuwa na sisi tunaitafuta sana elimu bila kujali kiwango cha elimu tuliyo nayo sasa, tuhakikishe kuwa maadamu tunaishi tunasoma hadi mwisho wa maisha yetu. Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye kuishi bila makuu licha ya ubunge wake. Hayo ni mambo ambayo sisi kama Vijana tunapaswa kuyaiga toka kwa marehemu Amina na kuyaenzi yale yote aliyoyaacha kwetu.

Wiki hii katika makala yangu, nilipanga kuandika tena juu ya suala la dawa za kulevya hasa ukizingatia kuwa ilikuwa ni wiki ya maadhimisho ya kupiga vita na kudhibiti matumizi ya dawa hizo. Hata hivyo suala la hilo nililiacha baada ya kusikia habari za msiba huu wa kusikitisha wa Mpendwa wetu Amina Chifupa Mpakanjia (Mbunge wa Vijana), sijui kama wengi tunalifahamu hili, lakini ni kuwa Marehemu Amina alikuwa anapigania sana suala la athari za matumizi ya dawa za kulevya kwa Vijana. Kwa neema, Mungu amemchukua Amina siku ya kilele cha kupambana na dawa za kulevya na siku hiyo (26.06.07), Mhe. Rais Jakaya Kikwete alikuwa Mjini Tanga kwenye maadhimisho ya siku hiyo ya kupambana na dawa hizo za kulevya. Hivyo Amina alikuwa ni Mpiganaji wa kweli katika tatizo hili, na hata Mungu anajua.

Mwanaharakati wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, marehemu Steve Biko aliyeuwawa kinyama na makaburu mwaka 1978 akiwa kijana mdogo, alikufa akiwa na falsafa hii, “HERI KUFA UKIWA NA KAULI INAYOISHI; KULIKO KUISHI UKIWA HUNA KAULI!”. Nimeikumbuka falsafa hii baada ya kifo cha Mhe. Amina. Ni kweli kuwa Amina amekufa, Amina amelala na wala hatutakaa tumuone tena katika maisha ya kibinadamu, lakini kauli zake zinaishi na kauli hizi zitaishi hata mwisho wa dunia. Hivyo Mpendwa Amina ninapenda kusema, VIJANA TULIKUPENDA, LAKINI MUNGU ALIKUPENDA ZAIDI, NENDA KAPUMZIKE DADA, LAKINI FAHAMU KUWA SISI KAMA VIJANA NA WANAJAMII TUNAKUMBUKA NA KUENZI MAMBO YOTE MAZURI ULIYOYAACHA!

Msahafu wa Kikristo (Biblia) unassema, “MTU AWAYE YOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO, BALI UWE KIELELEZO KWAO WAAMINIO, KATIKA USEMI, KATIKA MWENENDO, KATIKA UPENDO, NA KATIK AIMANI NA USAFI! –2 Timotheo 4:12–13.

Kweli Amina umelinda heshima ya Ujana wako na ndio maana sisi tunasema kuwa, tumejifunza kutoka kwako kuwa, kuishi bila kauli ni mbaya, heri kufa ukiwa na kauli inayoishi. Mwenyezi Mungu aipumzishe Roho yako mahali pema peponi, Upumzike kwa Amani.

Mungu Ibariki Tanzania! Mungu wabariki Vijana wa Tanzania!

Hillary N. Mkony,
Mwanaharakati wa masuala ya Vijana,
S.L.P. 743, Simu: 0754 000 215,
ARUSHA.

BURIANI AMINA CHIFUPA; VIJANA TUMEKUSIKIA!



Wiki hii taifa la Tanzania hususan jamii ya Vijana lilikumbwa na msiba mzito wa kuondokewa na Mbunge wa Viti Maalum (UV-CCM), Mhe. Amina Chifupa Mpakanjia aliyefariki tarehe 26.06.2007, baada ya kuugua kwa muda mfupi. Kimsingi msiba huu ni pigo kubwa sana kwa wanajamii wote na hasa sisi tulio katika mapambano ya kuwakomboa Vijana.

Mhe. Amina tulifahamiana kwa muda mfupi sana lakini kwa kipindi hicho kifupi, niligundua ni mtu mwenye msimamo usioyumba. Mwezi July, mwaka jana, niliandika makala kwenye gazeti hili juu ya Amina makala iliyokuwa na kichwa: “HONGERA MHE. CHIFUPA; WABUNGE WENGINE VIJANA MPO WAPI?” Baada ya makala hiyo nilipokea simu toka kwa waheshimiwa wabunge na mawaziri mbalimbali akiwemo Marehemu Amina mwenyewe, tulizungumza mengi na kuweza kuonana na tokea hapo, ndipo tulipozidi kuwa na ukaribu ulionifanya niweze kumfahamu Mhe.Amina kwa kiasi fulani.

Kwa kipindi kifupi nilichomfahamu Marehemu Amina, kimsingi nilijifunza mengi, hivyo leo nina ujasiri wa kumuandika na kusema kweli safari yake fupi hapa duniani haikuwa ni ya hasara, Marehemu Amina ameondoka kijasiri, Amekufa kishujaa. Amina amelala lakini bado fikra, mwelekeo, malengo, na kauli zake bado zinaishi na zitaishi milele yote. Ninakumbuka wakati alipokuwa anagombea Ubunge kupitia Jumuiya ya Vijana (UVCCM), jinsi ambavyo alikumbana na vikwazo mbalimbali kutoka kwa watu tofauti, wengine walidiriki hata kumuandika kwenye vyombo vya habari waziwazi wakimbeza na kumkashifu kuwa hafai kuwa mbunge, lakini yeye alisimama kidete na kulinda heshima na hadhi yake na hatimaye alifanikiwa kuvuka vikwazo hivyo na kuwa Mbunge mwenye umri mdogo kuliko wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata baada ya kuingia bungeni, Mhe Amina hakuwa kimya kama wengi walivyodhani, bali alisimama imara na kuonesha wazi nia na wajibu uliompeleka bungeni wa kuwatetea Vijana. Hivyo leo tunasikia Amina amefariki, tunajua wazi kuwa Vijana tumempoteza mwakilishi wetu hodari na aliyekuwa na nia ya kutusaidia.

Uwakilishi wa Mhe. Amina haukuishia kuchangia mijadala kwenye vikao vya Bunge tu, bado tulimsikia na kumuona akifanya shughuli mbalimbali za kijamii, kama kuwatembea vijana na watoto wenye matatizo mbalimbali, kwa hili tuliona jinsi Mhe. Amina alivyokuwa na moyo wa kuwatumikia Vijana na wanajamii wa Kitanzania.

Pamoja na kumkumbuka Mhe. Amina, ni vema sisi kama Vijana na wanajamii tukajiuliza ni kitu gani tumejifunza kutoka kwake, je ni jambo gani tutakalomkumbuka nalo maishani mwetu. Mimi binafsi kama Mwanaharakati na mdau wa masuala ya Vijana, nimejifunza mambo mengi kutoka kwa marehemu Amina na mambo hayo ni chamamoto kubwa kwangu katika wajibu na nafasi yangu ya kuwatumikia Vijana. Ninaomba niwakumbushe vijana na wanajamii mambo machache niliyojifunza kutoka kwa Mpendwa wetu huyu.

Amina alikuwa ni mwanaharakati, mpambanaji na mwakilishi mwenye nia na mikakati mingi na mizuri kwa ajili ya vijana siku za mbeleni. Mapambano ya Amina dhidi ya matatizo ya vijana na hususan suala la matumizi ya dawa za kulevya ni sehemu tu ya vitu ambavyo vilimjengea heshima kubwa kwa jamii na vijana na wote wenye mapenzi mema na maisha ya vijana hapa nchini. Ninakumbuka alisema kuwa yupo tayari kufa kwa ajili ya kuwatetea vijana wanaokabiliwa na matatizo mengi ya ukosefu wa kazi, elimu duni, ukosefu wa maeneo huru ya kufanyia biashara na suala la mmomonyoko wa maadili.

Marehemu Amina alikuwa ni kijana mwenye nia na malengo ya kufika mbali, hii ni pamoja na kusimama kwake kidete akilinda na kutetea nafasi yake kwa wale wote waliokuwa na nia ya kumkwamisha na kumrudisha nyuma, Amina alifahamu umuhimu wa elimu na ndio maana mpaka wakati anafariki licha ya kuwa alikuwa ni Mbunge, bado alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).

Mambo haya na mengine mengi yanamfanya Amina awe kioo kwetu kama Vijana na wanajamii wengine. Ninapenda kuwakumbusha wapendwa kuwa, katika kumuenzi na kumkumbuka Marehemu Amina ni wajibu wetu kusimama katika mstari ule aliosimama na kuutetea siku zote. Kwa waheshimiwa wabunge hususan wabunge vijana, mnapaswa kufahamu kuwa mna wajibu mzito wa kuwatetea vijana wenzenu bungeni na pia katika maeneo mbalimbali mnayoweza kuyafikia. Zaidi kuzidisha mapambano juu ya tatizo la dawa za kulevya ili vita hii ambayo Mhe. Amina aliipigania hadi siku ya umauti wake iweze kushinda na vijana wakombolewe katika hilo.

Kwa wapendwa vijana wenzangu, Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye ujasiri wa kupigania haki yake na hadhi aliyonayo kijamii, hivyo ni wajibu wetu leo kama Vijana kuhakikisha kuwa na sisi tunatetea na kulinda hadhi yetu kijamii, hadhi hii inapaswa kulindwa hata ikibidi kufa, lakini tusikubali mtu awaye yote atudhalilishe na kutudharau eti kwa kuwa sisi ni vijana. Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye kutafuta elimu, hivyo ni wajibu na nafasi yetu kama vijana kuhakikisha kuwa na sisi tunaitafuta sana elimu bila kujali kiwango cha elimu tuliyo nayo sasa, tuhakikishe kuwa maadamu tunaishi tunasoma hadi mwisho wa maisha yetu. Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye kuishi bila makuu licha ya ubunge wake. Hayo ni mambo ambayo sisi kama Vijana tunapaswa kuyaiga toka kwa marehemu Amina na kuyaenzi yale yote aliyoyaacha kwetu.

Wiki hii katika makala yangu, nilipanga kuandika tena juu ya suala la dawa za kulevya hasa ukizingatia kuwa ilikuwa ni wiki ya maadhimisho ya kupiga vita na kudhibiti matumizi ya dawa hizo. Hata hivyo suala la hilo nililiacha baada ya kusikia habari za msiba huu wa kusikitisha wa Mpendwa wetu Amina Chifupa Mpakanjia (Mbunge wa Vijana), sijui kama wengi tunalifahamu hili, lakini ni kuwa Marehemu Amina alikuwa anapigania sana suala la athari za matumizi ya dawa za kulevya kwa Vijana. Kwa neema, Mungu amemchukua Amina siku ya kilele cha kupambana na dawa za kulevya na siku hiyo (26.06.07), Mhe. Rais Jakaya Kikwete alikuwa Mjini Tanga kwenye maadhimisho ya siku hiyo ya kupambana na dawa hizo za kulevya. Hivyo Amina alikuwa ni Mpiganaji wa kweli katika tatizo hili, na hata Mungu anajua.

Mwanaharakati wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, marehemu Steve Biko aliyeuwawa kinyama na makaburu mwaka 1978 akiwa kijana mdogo, alikufa akiwa na falsafa hii, “HERI KUFA UKIWA NA KAULI INAYOISHI; KULIKO KUISHI UKIWA HUNA KAULI!”. Nimeikumbuka falsafa hii baada ya kifo cha Mhe. Amina. Ni kweli kuwa Amina amekufa, Amina amelala na wala hatutakaa tumuone tena katika maisha ya kibinadamu, lakini kauli zake zinaishi na kauli hizi zitaishi hata mwisho wa dunia. Hivyo Mpendwa Amina ninapenda kusema, VIJANA TULIKUPENDA, LAKINI MUNGU ALIKUPENDA ZAIDI, NENDA KAPUMZIKE DADA, LAKINI FAHAMU KUWA SISI KAMA VIJANA NA WANAJAMII TUNAKUMBUKA NA KUENZI MAMBO YOTE MAZURI ULIYOYAACHA!

Msahafu wa Kikristo (Biblia) unassema, “MTU AWAYE YOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO, BALI UWE KIELELEZO KWAO WAAMINIO, KATIKA USEMI, KATIKA MWENENDO, KATIKA UPENDO, NA KATIK AIMANI NA USAFI! –2 Timotheo 4:12–13.

Kweli Amina umelinda heshima ya Ujana wako na ndio maana sisi tunasema kuwa, tumejifunza kutoka kwako kuwa, kuishi bila kauli ni mbaya, heri kufa ukiwa na kauli inayoishi. Mwenyezi Mungu aipumzishe Roho yako mahali pema peponi, Upumzike kwa Amani.

Mungu Ibariki Tanzania! Mungu wabariki Vijana wa Tanzania!

Hillary N. Mkony,
Mwanaharakati wa masuala ya Vijana,
S.L.P. 743, Simu: 0754 000 215,
ARUSHA.

BURIANI AMINA CHIFUPA; VIJANA TUMEKUSIKIA!



Wiki hii taifa la Tanzania hususan jamii ya Vijana lilikumbwa na msiba mzito wa kuondokewa na Mbunge wa Viti Maalum (UV-CCM), Mhe. Amina Chifupa Mpakanjia aliyefariki tarehe 26.06.2007, baada ya kuugua kwa muda mfupi. Kimsingi msiba huu ni pigo kubwa sana kwa wanajamii wote na hasa sisi tulio katika mapambano ya kuwakomboa Vijana.

Mhe. Amina tulifahamiana kwa muda mfupi sana lakini kwa kipindi hicho kifupi, niligundua ni mtu mwenye msimamo usioyumba. Mwezi July, mwaka jana, niliandika makala kwenye gazeti hili juu ya Amina makala iliyokuwa na kichwa: “HONGERA MHE. CHIFUPA; WABUNGE WENGINE VIJANA MPO WAPI?” Baada ya makala hiyo nilipokea simu toka kwa waheshimiwa wabunge na mawaziri mbalimbali akiwemo Marehemu Amina mwenyewe, tulizungumza mengi na kuweza kuonana na tokea hapo, ndipo tulipozidi kuwa na ukaribu ulionifanya niweze kumfahamu Mhe.Amina kwa kiasi fulani.

Kwa kipindi kifupi nilichomfahamu Marehemu Amina, kimsingi nilijifunza mengi, hivyo leo nina ujasiri wa kumuandika na kusema kweli safari yake fupi hapa duniani haikuwa ni ya hasara, Marehemu Amina ameondoka kijasiri, Amekufa kishujaa. Amina amelala lakini bado fikra, mwelekeo, malengo, na kauli zake bado zinaishi na zitaishi milele yote. Ninakumbuka wakati alipokuwa anagombea Ubunge kupitia Jumuiya ya Vijana (UVCCM), jinsi ambavyo alikumbana na vikwazo mbalimbali kutoka kwa watu tofauti, wengine walidiriki hata kumuandika kwenye vyombo vya habari waziwazi wakimbeza na kumkashifu kuwa hafai kuwa mbunge, lakini yeye alisimama kidete na kulinda heshima na hadhi yake na hatimaye alifanikiwa kuvuka vikwazo hivyo na kuwa Mbunge mwenye umri mdogo kuliko wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata baada ya kuingia bungeni, Mhe Amina hakuwa kimya kama wengi walivyodhani, bali alisimama imara na kuonesha wazi nia na wajibu uliompeleka bungeni wa kuwatetea Vijana. Hivyo leo tunasikia Amina amefariki, tunajua wazi kuwa Vijana tumempoteza mwakilishi wetu hodari na aliyekuwa na nia ya kutusaidia.

Uwakilishi wa Mhe. Amina haukuishia kuchangia mijadala kwenye vikao vya Bunge tu, bado tulimsikia na kumuona akifanya shughuli mbalimbali za kijamii, kama kuwatembea vijana na watoto wenye matatizo mbalimbali, kwa hili tuliona jinsi Mhe. Amina alivyokuwa na moyo wa kuwatumikia Vijana na wanajamii wa Kitanzania.

Pamoja na kumkumbuka Mhe. Amina, ni vema sisi kama Vijana na wanajamii tukajiuliza ni kitu gani tumejifunza kutoka kwake, je ni jambo gani tutakalomkumbuka nalo maishani mwetu. Mimi binafsi kama Mwanaharakati na mdau wa masuala ya Vijana, nimejifunza mambo mengi kutoka kwa marehemu Amina na mambo hayo ni chamamoto kubwa kwangu katika wajibu na nafasi yangu ya kuwatumikia Vijana. Ninaomba niwakumbushe vijana na wanajamii mambo machache niliyojifunza kutoka kwa Mpendwa wetu huyu.

Amina alikuwa ni mwanaharakati, mpambanaji na mwakilishi mwenye nia na mikakati mingi na mizuri kwa ajili ya vijana siku za mbeleni. Mapambano ya Amina dhidi ya matatizo ya vijana na hususan suala la matumizi ya dawa za kulevya ni sehemu tu ya vitu ambavyo vilimjengea heshima kubwa kwa jamii na vijana na wote wenye mapenzi mema na maisha ya vijana hapa nchini. Ninakumbuka alisema kuwa yupo tayari kufa kwa ajili ya kuwatetea vijana wanaokabiliwa na matatizo mengi ya ukosefu wa kazi, elimu duni, ukosefu wa maeneo huru ya kufanyia biashara na suala la mmomonyoko wa maadili.

Marehemu Amina alikuwa ni kijana mwenye nia na malengo ya kufika mbali, hii ni pamoja na kusimama kwake kidete akilinda na kutetea nafasi yake kwa wale wote waliokuwa na nia ya kumkwamisha na kumrudisha nyuma, Amina alifahamu umuhimu wa elimu na ndio maana mpaka wakati anafariki licha ya kuwa alikuwa ni Mbunge, bado alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).

Mambo haya na mengine mengi yanamfanya Amina awe kioo kwetu kama Vijana na wanajamii wengine. Ninapenda kuwakumbusha wapendwa kuwa, katika kumuenzi na kumkumbuka Marehemu Amina ni wajibu wetu kusimama katika mstari ule aliosimama na kuutetea siku zote. Kwa waheshimiwa wabunge hususan wabunge vijana, mnapaswa kufahamu kuwa mna wajibu mzito wa kuwatetea vijana wenzenu bungeni na pia katika maeneo mbalimbali mnayoweza kuyafikia. Zaidi kuzidisha mapambano juu ya tatizo la dawa za kulevya ili vita hii ambayo Mhe. Amina aliipigania hadi siku ya umauti wake iweze kushinda na vijana wakombolewe katika hilo.

Kwa wapendwa vijana wenzangu, Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye ujasiri wa kupigania haki yake na hadhi aliyonayo kijamii, hivyo ni wajibu wetu leo kama Vijana kuhakikisha kuwa na sisi tunatetea na kulinda hadhi yetu kijamii, hadhi hii inapaswa kulindwa hata ikibidi kufa, lakini tusikubali mtu awaye yote atudhalilishe na kutudharau eti kwa kuwa sisi ni vijana. Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye kutafuta elimu, hivyo ni wajibu na nafasi yetu kama vijana kuhakikisha kuwa na sisi tunaitafuta sana elimu bila kujali kiwango cha elimu tuliyo nayo sasa, tuhakikishe kuwa maadamu tunaishi tunasoma hadi mwisho wa maisha yetu. Mhe. Amina alikuwa ni mtu mwenye kuishi bila makuu licha ya ubunge wake. Hayo ni mambo ambayo sisi kama Vijana tunapaswa kuyaiga toka kwa marehemu Amina na kuyaenzi yale yote aliyoyaacha kwetu.

Wiki hii katika makala yangu, nilipanga kuandika tena juu ya suala la dawa za kulevya hasa ukizingatia kuwa ilikuwa ni wiki ya maadhimisho ya kupiga vita na kudhibiti matumizi ya dawa hizo. Hata hivyo suala la hilo nililiacha baada ya kusikia habari za msiba huu wa kusikitisha wa Mpendwa wetu Amina Chifupa Mpakanjia (Mbunge wa Vijana), sijui kama wengi tunalifahamu hili, lakini ni kuwa Marehemu Amina alikuwa anapigania sana suala la athari za matumizi ya dawa za kulevya kwa Vijana. Kwa neema, Mungu amemchukua Amina siku ya kilele cha kupambana na dawa za kulevya na siku hiyo (26.06.07), Mhe. Rais Jakaya Kikwete alikuwa Mjini Tanga kwenye maadhimisho ya siku hiyo ya kupambana na dawa hizo za kulevya. Hivyo Amina alikuwa ni Mpiganaji wa kweli katika tatizo hili, na hata Mungu anajua.

Mwanaharakati wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, marehemu Steve Biko aliyeuwawa kinyama na makaburu mwaka 1978 akiwa kijana mdogo, alikufa akiwa na falsafa hii, “HERI KUFA UKIWA NA KAULI INAYOISHI; KULIKO KUISHI UKIWA HUNA KAULI!”. Nimeikumbuka falsafa hii baada ya kifo cha Mhe. Amina. Ni kweli kuwa Amina amekufa, Amina amelala na wala hatutakaa tumuone tena katika maisha ya kibinadamu, lakini kauli zake zinaishi na kauli hizi zitaishi hata mwisho wa dunia. Hivyo Mpendwa Amina ninapenda kusema, VIJANA TULIKUPENDA, LAKINI MUNGU ALIKUPENDA ZAIDI, NENDA KAPUMZIKE DADA, LAKINI FAHAMU KUWA SISI KAMA VIJANA NA WANAJAMII TUNAKUMBUKA NA KUENZI MAMBO YOTE MAZURI ULIYOYAACHA!

Msahafu wa Kikristo (Biblia) unassema, “MTU AWAYE YOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO, BALI UWE KIELELEZO KWAO WAAMINIO, KATIKA USEMI, KATIKA MWENENDO, KATIKA UPENDO, NA KATIK AIMANI NA USAFI! –2 Timotheo 4:12–13.

Kweli Amina umelinda heshima ya Ujana wako na ndio maana sisi tunasema kuwa, tumejifunza kutoka kwako kuwa, kuishi bila kauli ni mbaya, heri kufa ukiwa na kauli inayoishi. Mwenyezi Mungu aipumzishe Roho yako mahali pema peponi, Upumzike kwa Amani.

Mungu Ibariki Tanzania! Mungu wabariki Vijana wa Tanzania!

Hillary N. Mkony,
Mwanaharakati wa masuala ya Vijana,
S.L.P. 743, Simu: 0754 000 215,
ARUSHA.

"MHESHIMIWA KIKWETE; VIJANA WANASEMA HIVI ..........."


Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Naomba leo nitumie nafasi na ukurasa huu wa Kona ya Vijana kuzungumza nawe juu ya mambo machache ambayo nimekuwasikia vijana wanayazunguza na kutamani kuyafikisha kwako juu ya serikali yako na namna wanavyokutazama katika nafasi yako juu ya mustakabali wa maisha yao chini ya jua hili. Hivyo ninaomba ufahamu kuwa vijana wengi wana mengi ya kusema nawe kama ilivyo kwa watanzania wengi, tatizo kubwa ni namna ya kufikisha kauli yao hiyo kwako. Hivyo mimi naomba nibebe wajibu huo wa kuwa kipaza sauti cha vijana kwa kufikisha kauli yao kwako.

Awali ya yote napenda kukupa pole kutokana na majukumu mengi ya kuwatumikia watanzania, majukumu uliyokabidhiwa na wananchi kupitia sanduku la kura mnano tarehe 14.12.2005. Mungu akuwezeshe kuyatekeleza kwa faida ya watanzania walioonyesha matumaini na matarajio makubwa juu yako. Kila la kheri.

Mheshimiwa Rais, tarehe 12.08. kila mwaka Tanzania itaungana na mataifa mengine duniani katika kuadhimisha wiki ya kimataifa ya Vijana ambayo imekuwa ikiadhimishwa kila mwaka kwa makundi mbalimbali ya vijana na wadau mbalimbali wa masuala ya vijana kukutana katika maeneo tofauti na kuzungumza juu ya mambo tofauti juu ya vijana. Sina uhakika mwaka huu maadhimisho hayo kitaifa yatafanyika wapi kwani mpaka sasa, wizara inayohusika haijaweka wazi ni wapi jukumu hilo litafanyika. Hata hivyo, hayo hayatanifanya mimi kama mdau na mwanaharakati wa vijana kuacha kutimiza wajibu wangu wa kuwasemea vijana. Kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho hayo inasema, “ONEKANA: SIKIKA, USHIRIKI WA VIJANA KWA MAENDELEO”! Hivyo ni wajibu wetu kama vijana na wanajamii kutafuta namna ya kuwafikia vijana katika siku hii muhimu ya maadhimisho hayo kimataifa.

Mheshimiwa Rais, kwa muda mrefu sasa vijana wa kitanzania wamekuwa wakilalamika juu ya mazingira magumu yanayowakabili katika harakati zao za kimaisha. Hii inatokana na jinsio hali ilivyobadilika tofauti na matarajio waliyokuwa nayo juu yako kabla na baada ya kuchaguliwa kwako kuwa rais wa awamu ya nne wa Tanzania. Hivyo wamekuwa wakijiuliza kama ni kweli kuwa ile kauli ya “Maisha bora kwa kila Mtanzania” na ile ya “Tanzania yenye neema yawezekana” inawahusu wao au ni kwa wale wachache tu walio katika mazingira ya kujichukulia Chao Mapema. Ninakumbuka wakati unapiga kampeni na kuomba kura kwa watanzania ulikuwa na kauli mbiu nzuri juu ya vijana kuwa utawawezesha Vijana kujiajiri na pia utatoa nafasi za ajira kwa vijana milioni moja kwa mwaka, hivyo kwa miaka mitano ya mwanzo ya serikali yako, zingepatikana nafasi za ajira milioni tano. Kauli mbiu hizo pamoja na nyingine nyingi ndizo zilizokuwezesha wewe kupata ushindi mkubwa uliotingisha na kuuita Ushindi wa Tsunami.

Mheshimiwa Rais, wakati uliporudi jijini Dar es salaam baada ya kuteuliwa Mjini Dodoma kwako kuwa mgombea wa CCM katika uchaguzi mkuu wa 2005, ulipata mapokezi makubwa sana ambapo pamoja na mambo mengine ulikutana na kilio cha vijana juu ya matatizo mbalimbali yanayowakabili. Hivyo walipoongea nawe katika Ukumbi wa Diamond Jubelee ulisema kuwa umesikia kilio chao na hivyo uliahidi kujitahidi kutafuta namna ya kuwasaidia vijana hao kutoka katika hali ngumu ya maisha inayowakabili. Hata hivyo hali imekuwa ni tofauti na matarajio yao ndani ya miezi kumi na nane tangu serikali yako iingie madarakani. Swali la vijana ni je ulikuwa unawalaghai au kuna vitu ulivyokutana navyo ikulu vikakwamisha dhamira yako njema uliyokuwa nayo dhidi yao? Swali hili limekuwa likiulizwa kwani mambo yanayoendelea kwa vijana baada ya kuingia madarakani serikali yako yamewakatisha tamaa na wengi wamekuwa wakijuta kwani hawakutarajia kuona hayo hasa kwa kuzingatia kuwa eti (ulikuwa mshikaji wao) katika hali ngumu ya maisha. Vijana wamekuwa wakiuliza kuwa je zile ajira milioni moja ulizoahidi kila mwaka bado zipo au zinachukuliwa na wawekezaji wa nje au ni kwa vijana wapi, na kwa wale uliowaahidi kuwawezesha kujiajiri ni hao serikali yao iliyoamua kuwafukuza mjini kwa kuwa wanachafua miji kwa kutembeza bidhaa mikononi na kuuza mitumba katika maeneo ambayo mnadai si maeneo ambayo si rasmi? Je ni wapi mlipowatengea vijana hao penye nafasi na miundo mbinu bora na wakakataa kwenda?

Mheshimiwa Rais, hivi karibuni nilikuwa jijini Dar es salaam, ambapo kwa bahati nzuri nilipata nafasi ya kuzunguka katika maeneo mengi ya jiji hilo, kwa sehemu kuwa vijana waliokuwa wakifanya biahsar zao za kuuza mitumba na bidhaa nyingine (maarufu kama wamachinga), wameondolewa na kupelekwa katika maeneo yasiyo na biashara wala miundo mbinu, matokeo yake wengi wamekata mitaji yao kiasi cha baadhi yao kuamua kujiua baada ya kubomolewa kwa vibanda vyao bila kujua kama huko walipokuwa wanapelekwa ni sehemu sahihi au la. Zoezi hilo limehamia pia kwa wapiga debe na makondakta wasio na shughuli maalum katika vituo mbalimbali vya daladala. Hata hivyo licha ya hatua hiyo kuchukuliwa kwa ajili ya vijana hao ambao nao ni wahitaji na wamekuwa wakitegemea kupata riziki kupitia maeneo hayo, bado hakuna hatua mbadala zimechukuliwa katika kuwasaidia wahusika hao ili wasiende kufanya zile biashara za kutegemea mtaji wa nguvu zao (wizi, ujambazi, umalaya na ukahaba). Zoezi hili si la jijini Dar es salaam tu, bali ni katika maeneo yote ya nchi yetu. Kwa sehemu kubwa inaonekana kuwa tumehamisha tatizo tkutoka sehemu moja na kulipeleka sehemu nyingine, kwani hakuna mbinu mbadala za kuwasaidia hao tuliowaondoa mjini. Mfano ulio hao ni wale wote waliokuwa wakifanya biashara ya ukahaba na uchangudoa pale Manzese, nasikia wamahamishia biashara yao pale Buguruni na wanafanya biashara yao hadharani bila woga wowote.

Mheshimiwa Rais, mwaka jana serikali yako ilitenga kiasi cha shilingi bilioni moja kwa kila mkoa ili kuweza kuwakopesha wajasiriamali wadogo, hata hivyo mpaka sasa ninapokuandikia barua hii, kwa kweli fedha hizo zimeishia mifukoni mwa watu wachache tu tena wale walio na mitaji na fedha, vijana na wananchi wengi wa chini, hakuna hata mmoja aliyepata mikopo hiyo. Sasa tunajiuliza kama ni kweli serikali yako ilikuwa makini juu ya hilo au bado hali ni ile ile ya kuwabeba wale walio nacho na wale wasio nacho hata ile mitaji yao midogo wananyang’anywa kwa kuwabomolea vibanda vyao na kuchukua mitumba yao na vyakula vya akina mama ntilie? Hili unaweza kulithibisha kwa kufanya ziara katika mabenki na vyombo vyote vilivyopewa dhamana ya kutoa mikopo hiyo. Kwa hali hii vijana wanauliza kama kweli wewe ndie waliyekuwa wanakutarajia au bado wamatarajie mwingine ajaye?

Mheshimiwa Rais, pamoja na kauli nzuri za viongozi wetu juu ya kuwataka vijana kurudi vijijini kwa ajili ya kujiingiza katika kilimo na ufugaji lakini ukipita katika maeneo mengi ya vijijini utakutana na hali mbaya ya maisha ya huko na wala hakuna miundo mbinu mizuri wala pembejeo kwa wale wote wanaoamua kujikita katika sekta hizo muhimu. Na kwa wale wachache wanaojifanyia shughuli hizo, bado hawapati soko wala mazao yao hayanunuliwi kwa wakati na kama wanauza mazao yao basi ni kwa wafanyabiashara ambao wananunua mazao hayo kwa bei ya chini na hivyo kuwa ni hasara kwao. Nani atawasaidia hao katika mikakati yao ya kujikwamua kiuchumi? Wakati ninaandika barua hii nikakumbuka juu ya kashfa iliyomkumba mbunge mmoja aliyekopa mabilioni ya fedha katika benki moja kwa dhamana ya serikali huku wajasiriamali wadogo wakikosa fursa hiyo, pia kuna taarifa ya mbunge mwingine aliyekiri kuwa yeye anamiliki benki hapa nchini na huku mbunge mwingine aliyepewa kibali cha kujenga Hoteli ya Kitalii kwenye eneo ambalo haliruhusiwi kwani itaathiri mazingira ya bahari lakini akapewa kibali tu. Hapo pia vijana wanauliza, mbona wao hata kama wamejiunga katika vikundi vya watu wasiopungua hamsini wanawezi kupata mikopo ili nao wafanye biashara zitakazowanyanyua kiuchumi na hivyo kuitwa wajasiriamali wa ndani? Kwa hili unasemaje mheshimiwa rais?

Mheshimiwa Rais, vitendo vya unyanyasaji na kuwaua vijana na wachimbaji wadogo vinavyofanywa na wachimbaji wakubwa ambao wengi si raia katika maeneo mbalimbali ya migodi ya madini yetu ni sehemu ya kilio cha kila mara huku serikali yako ikifumbia macho bila kutoa walao kauli ya kukemea matendo hayo ni sehemu ya swali ambalo vijana wamekuwa wakiuliza. Wao wana nafasi na kauli gani katika kujinufaisha na ujtajiri huo ambao ni sehemu ya neema kubwa Mwenyezi Mungu aliyoitunukia Tanzania na sasa inachukuliwa na wageni kama mali isiyo na wenyewe? Ni vema ukawajibu vijana hata hili.

Mheshimiwa Rais, hivi karibuni ulioongoza watanzania katika kampeni ya upimaji wa hiari wa VVU/UKIMWI. Kimsingi ninakupongeza sana kwa hatua hiyo muhimu uliyoichukua, hasa baada ya kuungwa mkono na baadhi ya wabunge wakiongozwa na Spika wa Bunge, Mhe. Samwel Sitta na Waziri Mkuu, Mhe. Edward Lowassa na wake zao. Hata hivyo bado ni lazima tujiulize kama hatua hii ni ya kitaalamu au ni ya kisiasa zaidi. Pmaoja na hayo ni vema serikali pia ikawa na msaada kwa wale wote walioamua kuwa wazi baada ya kuthibitika kuwa wanaishi na VVU. Nina fahamu juu ya vikundi mbalimbali vya vijana katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu wanaoishi na VVU, lakini pamoja na wao kukaa kama familia, bado hawapati misaada itakayowawezesha walao kuwa na miradi ya kuwapatia mapato ili waweze kujikimu kimaisha kwani iwapo vijana hawa wasipopata misaada hivyo, ni hatari sana kwa maisha ya watanzania wengine kwani wanaweza kuamua kusambaza VVU kwa makusudi bila kujulikana kwani licha ya kuwa wamekuwa wazi kuwa wanaishi na VVU, wengi wao wamekuwa wakitongozwa na wanaume/wanawake wengine kwa kuwa hawajionyeshi na kwa kweli wengi wao ni wazuri wa sura na miili na afya zao ni nzuri na wala huwezi kuwatilia shaka kama hutaelezwa kuwa wanaishi na VVU. Hili pia ni swali la vijana kwako.

Mheshimiwa Rais, nina mengi ya kuzungumza nawe kwa niaba ya vijana wa Tanzania, hata hivyo naomba uniruhusu niseme kuwa umefika wakati wa kuwasiliza vijana, kwani kilio kikubwa cha vijana ni kutokusikilizwa. Hivyo ninakuomba sana ujitahidi pamoja na ratiba yako kutingwa na shughuli nyingi za nchi, utenge walao siku moja ili ukae na vijana wa Tanzania uwasikilize kwani nina imani kuwa wana mambo mengi ya kusema nawe. Ninayasema haya kwa kuwa mpaka sasa hakuna waziri yeyote wa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana aidha aliyekuwa Waziri Mhe. Prof. Jumanne Maghembe au wa sasa Mhe. John Chiligati au hata manaibu mawaziri wao, aliyewahi kupanga na kukaa na vijana na kuwasikiliza katika kilio chao. Fahamu kuwa kwa sehemu kubwa inawezeakana kuwa mengi huyafahamu na wala hujayasikia yote, lakini ukipata nafasi ya kuwasikiliza vijana utafahamu hayo na mengi zaidi ambayo ulikuwa hujayasikia.

Mheshimiwa Rais, nimalizie kwa kusema kuwa, vijana wanahitaji kusikia jambo jipya, wengi wanatamani kupata nabii mpya wa kuwaokoa na wala habari za kisiasa si za lazima kwao kwani wengi wana maisha magumu, hawajui watakula nini kesho na wala maisha yao watayaboresha vipi. Hivyo unaombwa kubeba wajibu huo kwa nguvu mpya ili vijana wakiri kuwa sasa wameuona ukombozi ulio tayari kwao. Ni matarajio ya vijana kusikia kitu juu ya hayo na mengine mengi ambayo hayajaandikwa hapa.

Mungu Ibariki Tanzania! Mungu wabariki Vijana wa Tanzania!

Mwanaharakati wa Masuala ya Vijana,

Hillary N. Mkony,
S.L.P. 743, Simu: 0754-000215,
Barua pepe: hillarymy@yahoo.com
ARUSHA.